UMEWAHI KUJIULIZA UKIFUTA VITU KWENYE KIFAA CHAKO HUWA VINAENDA WAPI?

 


"Marehemu Ruge aliwahi kusema Ogopa Mungu na Teknolojia"

Katika ulimwengu wa kidijitali, taarifa zako za kibinafsi zinaweza kuangukia mikononi mwa watu wasio waaminifu ikiwa taarifa au vitu vyako havijafutika kikamilifu kupitia simu au kompyuta.

Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2023 ya Shirika la Data Security Council of India, zaidi ya asilimia 40 ya vifaa vilivyotupwa bila kufutwa data kikamilifu vilikuwa na taarifa za siri za watumiaji, jambo ambalo linaweza kusababisha uhalifu wa mtandaoni.

Je, Umewahi Kufikiria Vitu Unavyofuta Kwenye Kifaa Chako Huenda Wapi?

Wataalamu wa teknolojia wanasema, hakuna kitu kinafutika ulimwenguni hasa katika upande wa teknolojia ...

Yaani kivipi? Mfano umepiga picha ya kitu ukasema umekifuta kwenye simu yako, picha hiyo haiwezi kuonekana tena, lakini bado inahifadhiwa kwenye hifadhi ya ndani ya kifaa chako, unaambiwa wataalamu wa mambo wanauwezo wa kukirudisha endapo wakipata Access ya kifaa yako. Hii ndiyo sababu kuna programu maalumu zinazoweza kurejesha vitu vilivyofutwa.

Swali la kujiuliza kwa Nini Faili Hazifutiki Moja kwa Moja?

Sababu kuu ni ufanisi. Simu au Kompyuta yako haiondoi faili au data zilizofutwa moja kwa moja, kwa sababu mchakato huo unahitaji muda mrefu zaidi.

Badala yake nafasi inabaki wazi kwa matumizi mapya ya data nyingine. Njia hii pia inatoa fursa ya kurejesha vitu vilivyofutika kwa bahati mbaya.

Lakini hali hii ipo tofauti katika mfumo wa HDD yaani (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive).

Vitu vilivyofutwa kupitia HDD (HARD DISK DRIVE) vinaweza kurejeshwa kwa urahisi kwa kutumia programu za urejeshaji data.

Hata hivyo kupitia mfumo wa SSD (Solid State Drive), hali ni tofauti. SSD hutumia mchakato maalum unaoitwa TRIM, ambao unafuta data mara moja ili kuboresha kasi na ufanisi wa kifaa. Katika hatua nyingine, bado kuna hatari ya baadhi ya data kutofutika kikamilifu endapo haitosimamiwa kwa umakini.

Ikiwa unataka kuhakikisha kuwa vitu vyako vimefutwa kabisa na haviwezi kurejeshwa kupitia kifaa unachotumia, ni muhimu kutumia programu maalum za kufuta data kama vile Eraser, CCleaner, au Darik’s Boot and Nuke (DBAN).

Programu hizi hufanya kazi ya kuandika data mpya juu ya nafasi iliyoachwa wazi na vitu vilivyofutwa, na hivyo kufanya data za awali zisirejeshwe tena. Ili kuhakikisha usalama wa data zako, tumia mbinu za kitaalamu za kufuta data. Usalama wa taarifa zako ni jukumu lako.

Tafakari mara mbili kabla ya kufuta, kwa kufanya hivyo, utakuwa umelinda faragha yako na kuzuia uwezekano wa taarifa zako kutumiwa vibaya.

Post a Comment

0 Comments