Fikiria dunia ambayo utambulisho wako hauhitaji kadi, nywila au hata saini. Bali alama zako za vidole, sura au hata sauti yako. Hii si ndoto tena, bali ni hali halisi inayoendelea kushika kasi duniani, ikiendeshwa na teknolojia ya biometric.
Teknolojia hii imepata mafanikio makubwa, hususani nchini
China, ambayo imeunganishwa na mifumo ya kisasa kama kamera za usalama (CCTV)
na huduma za kidijitali. Mojawapo ya matumizi yake ni katika kuboresha
huduma za Social Credit System, mfumo unaolenga kupima
na kuboresha tabia za kijamii na kiuchumi za raia wake.
Mfumo huu hutumia taarifa za alama za vidole kuhakiki
utambulisho (BIOMETRIC) Kwa lengo la kupunguza udanganyifu, kurahisisha huduma
kuanzia ulipaji wa bidhaa mpaka manunuzi, pamoja na kuboresha usalama kwa umma.
Faida zake ni dhahiri zipo wazi, Wahenga wanasema kizuri
hakikosi kasoro licha ya mfumo huu kupata mafanikio bado unakumbwa na
changamoto hasa kwa mataifa yanayoendelea kama Tanzania.
Swali la kujiuliza, Je tuko tayari kuboresha mfumo huu au
tunahitaji muda zaidi?
Katika mazingira yetu, swali kubwa linalojitokeza ni usalama
wa taarifa za kibinafsi. Katika nchi nyingi zinazoendelea, mifumo ya kuhifadhi
na kulinda taarifa za kidijitali bado ni dhaifu, na mara nyingi haina uwazi wa
kutosha kuhusu jinsi data za watu zinavyotumika.
Je, tunayo miundombinu madhubuti ya kuhakikisha taarifa hizi
haziingiliwi na watu wenye nia mbaya, ikiwemo sheria na sera zinazolinda
faragha ya raia?
Kulingana na ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la
International Telecommunication Union (ITU) mwaka 2022, nchi nyingi
zinazoendelea bado zina safari ndefu kufikia kiwango kinachoridhisha cha
usalama wa data.
Hili linaibua mjadala mzito kuhusu uwezo wa mataifa haya
kushiriki kikamilifu katika mapinduzi ya teknolojia hii.
TUSIFANYE
HARAKA.
Ni kweli, teknolojia ya biometric inaweza kuwa nyenzo muhimu
ya maendeleo. Lakini je, tunapaswa kuikimbilia bila mpango madhubuti? Ili
teknolojia hii iwe na manufaa ya kweli, tunahitaji muda wa kujifunza, kuboresha
miundombinu yetu, na kuimarisha sera zinazolinda haki za watu.
Hii si hadithi ya kutisha, bali ni changamoto ya
kufikirisha. Dunia ya biometric hipo hapa, lakini swali ni moja, Je Tanzania
na mataifa mengine yanayoendelea yamejiandaa kuingia katika ulimwengu huu
pamoja na uwajibikaji unaohitajika? Ni
wakati wa kufanya maamuzi sahihi, si kwa haraka, bali kwa busara. Wakati
teknolojia ikisonga mbele, faragha ya binadamu lazima ibaki kuwa kipaumbele.

1 Comments
Thanks, good news👏
ReplyDelete